Mikoa mitano ya juu ilikuwa na uwiano mzuri wa mwalimu kwa wanafunzi katika shule za msingi mwaka 2015 na katika mtihani wa darasa la saba mwaka huo minne kati ya hiyo kasoro Iringa ilikuwa kwenye 10 bora. Mikoa mingine mitano ya mwisho ilikuwa na uwiano wa juu ya kiwango kinachotakiwa cha 1:40 na minne kati ya hiyo kasoro Geita ilikuwa kwenye orodha ya 10 ya mwisho katika mtihani wa darasa la saba.